Idadi kubwa ya watu inahofiwa imepoteza maisha kufuatia kuzama kwa meli iitwayo MV Spice ilokuwa ikitoka Unguja kwenda Pemba. Ajali hiyo ilitokea katika mkondo wa Nungwi unaojulikana kwa maji makali mwendo wa saa saba
usiku wa kuamkia leo.
Msajili wa meli wa zanzibar amesema
meli hiyo ilikuwa na leseni ya kubeba abiria 600 lakini wasi wasi
umekuwa mkubwa kwa vile meli za Unguja na Pemba hujaza bila kiasi.
Mpaka sasa watu wasiopungua 163 wamekufa, aidi ya watu 100 bado hawajulikani walipo,
lakini watu 325 walionusurika wameokolewa, kwa mujibu wa waziri wa
masuala ya dharura wa Zanzibar.
Shughuli ya uokoaji inaendelea hivi sasa na tayari serikali ya Zanzibar imeanza mipango ya kupokea maiti
Source: BBC Swahili

1 comment:
ni msiba mkubwa poleni wafiwa wote na wajerehiwa wote. mwenyezi mung awape nguvu kwa kipindi hiki kigumu.
Post a Comment